Most Popular

MATUKIO YA KISIASA

 

15.09.2016 

DRC: kalenda ya uchaguzi itaanza na uchaguzi wa urais

Uchaguzi wa rais, wa wabunge na wa mkoa utafanyika mbalimbali DRC.
 Ujumbe wa kambi ya upinzani ulikua unataka uchaguzi wa urais ndio uanze. Uchaguzi huo utafanyika na chaguzi zingine tatu ikiwa kifedha na kiufundi itawezekana.ENDELEA

 

10.09.2016

Washirika wa kisiasa wa Merkel wazidi kumtia kishindo 

 

Merkel, ambaye umaarufu wake wa muda mrefu umeshuka kufuatia mgogoro wa wakimbizi, siku ya Jumatano alivionya vyama vya siasa dhidi ya kujishusha hadhi kwa kuchukuwa msimamo wa chama cha AfD wa kueneza chuki dhidi ya Uislamu.ENDELEA

 

10.09.2016

Viongozi wa NATO, EU wazuru Uturuki 

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akisalimiana na katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg mjini Ankara.
 Uturuki imekuwa ikitaka kujiunga na Umoja wa Ulaya kwa muda mrefu, lakini imewatuhumu wazungu kwa kukwamisha mchakato huo kwa sababu ya chuki dhidi ya taifa hilo la Kiislamu. Maafisa wa Umoja wa Ulaya wanasema Uturuki bado haijatimiza masharti kuhusu haki za msingi na uhuru.ENDELEA

 

09.09.2016

Korea Kaskazini yafanya 'jaribio kubwa la nyuklia'

 

 Korea Kaskazini kufikia sasa haijasema lolote kuhusu jaribio hilo, lakini wachanganuzi wanasema hii huenda ikawa ishara ya hatua zilizopigwa na taifa hilo katika kustawisha teknolojia yake ya nyuklia.
Mitetemeko ya ardhi ya kusababishwa na binadamu ambayo imetokea eneo hilo awali yote ilitokana na majaribio ya nyuklia.ENDELEA

09.09.2016

Jean Ping wa Gabon kukata rufaa, mahakama ya rufaa

 

  Bwana Ping amesema watu kadhaa wameuawa kwenye vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi , lakini serikali imesema kuwa ni watatu pekee ndiyo waliuawa.ENDELEA

09.09.2016 

Obama:Trump hana ufahamu

 

Akizungumza Laos, Bw Obama amesema kuwa kila mara Bw Trump anapoongea inabainika kwazi kwamba mgombea wa Republican hafai kuwa rais.ENDELEA

 

07.09.2016

 

Rais Bongo awatuhumu waangalizi wa umoja wa Ulaya

 Akizungumza kupitia kituo cha taifa cha Redio cha RTL, Rais Bongo amesema kuwa, angetamani kuona waangalizi hao pia wanagusia kasoro zilizoshuhudiwa kwenye ngome za mpinzani wake wake, mjini Fiefdom.ENDELEA

07.09.2016

Amani yaanza kutengamaa Sudan Kusini

 Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Salva Kiir amemtumia ujumbe Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki akimuarifu kuwa hali ya usalama katika nchi hiyo imeanza kutengemaa.ENDELEA

 

05.09.2016

Merkel atikiswa uchaguzi mdogo Ujerumani

 

 Kansela wa Ujerumani,Angela Merkel ameonekana kutikiswa kisiasa huko kaskazini mashariki mwa jimbo la Mecklenburg-Pomerania.ENDELEA

 05.09.2016

Wataamu wasema wizi wa kura barani Afrika waelekea kukoma

 

 Wakati huu nchi ya Gabon ikikabiliwa na machafuko ya mara baada ya uchaguzi mkuu ulioshuhudia kurejea madarakani kwa Rais Ali Bongo Ondimba, wataalamu wanasema kuwa udanganyifu wa chaguzi barani Afrika unazidi kuwa mgumu, shukrani kwa mashirika ya kijamii ambayo yamekuwa yakifuatilia chaguzi mbalimbali na kukosoa pamoja na kuenea kwa teknolojia ya simu za mkononi.ENDELEA

  05.09.2016

Hakuna siri tena, Kenyatta asaini kuwa sheria muswada wa haki ya kupata taarifa

 Muswada wa haki ya kupata taarifa nchini Kenya wa mwaka 2015, hatimaye umetiwa saini na Rais kuwa sheria, ukiruhusu raia wa Kenya kupata taarifa kwa uhuru kutoka Serikalini pamoja na ofisi nyingine za uma.ENDELEA

 

05.09.2016

Obama na Xi Jinping waendelea kutofautiana kuhusu Bahari ya China Kusin

 Hata hivyo Rais Xi alipinga mpango wa Marekani wa kupeleka mfumo wa kuzuia makombora katika anga huko Korea Kusini. Aliitaka Marekani kuheshimu maslahi ya kimkakati na usalama ya China.
Kwa upande wake rais Obama wa Marekani alisisitiza kwamba nchi yake lazima ihakikishe usalama wa washirika wake.ENDELEA

 

04.09.2016

Rais Robert Mugabe atoa mzaha kuhusu afya yake

 

  Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amepuuzilia mbali taarifa za hivi karibu za uvumi juu ya afya yake, kwa kutoa mzaha kwamba alikufa na akafufuka.ENDELEA

04.09.2016

Kuapishwa rais mpya nchini Brazil katika anga ya mgogoro wa kisiasa na kiuchumi

Michel Temer, rais wa muda nchini Brazil amekula kiapo kama rais mpya wa nchi hiyo.
Mbali na Temer kuahidi kufanya juhudi kwa ajili ya kuokoa uchumi wa Brazil kutokana na mdororo, amesisitiza pia kwamba, hivi sasa na baada ya kuenguliwa madarakani Rais Dilma Rousseff, umefika wakati wa kuiunganisha nchi hiyo. Katika hotuba yake ya kwanza kwa taifa na baada ya kuapishwa,ENDELEA

 

04.09.2016

Uhuru akanusha mvutano kati ya Kenya na Tanzania

 

Akizungumza mjini Mombasa wakati wa ufunguzi gati la makontena katika bandari ya Mombasa, Kenyatta alipuuzia maneno kwamba kuna mvutano wowote na badala yake akasema kuwa nchi hizo zinasaidiana.ENDELEA

 

04.09.2016

Jean Ping ajitangaza rais nchini Gabon ataka kura kuhesabiwa upya

 Watu watano wameuawa na maelfu kukamatwa katika makabiliano kati ya wafuasi wa upinzani na jeshi la polisi jijini Libreville.ENDELEA

 

 

02.09.2016

Uzbekistan 'waomboleza kifo' cha rais Islam Karimov 

 

Watangazaji waandamizi wa runinga ya taifa na viongozi wakuu wa serikali nchini Uzbekistan wametuma ujumbe wa tanzia katika mitandao ya kijamii kufuatia kuzagaa kwa uvumi kuwa rais Islam Karimov ameaga dunia.ENDELEA

 

02.09.2016

Melania Trump ashtaki gazeti kuhusu tuhuma za ukahaba

 

 Melania Trump amelishtaki gazeti la Daily Mail la Uingereza pamoja na mwanablogu wa Marekani akitaka alipwe $150m (£114m) kuhusiana na tuhuma kwamba alikuwa kahaba miaka ya 1990, wakili wake amesema.ENDELEA

02.09.2016

Mamia ya watu wakamatwa katika vurugu Gabon

Ali Bongo

 

Rais Ali Bongo ambaye ndiye aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi huo amewalalamikia wafuasi wa upinzani ambao walimiminika mitaani siku ya Jumatano na kuchoma moto bunge la nchi hiyo.
Amesema demokrasia haiwezi kupatikana kwa njia kama hizo.ENDELEA

 

01.09.2016

Hatimaye Rousseff aenguliwa rasmi madarakan

Dilma Rousseff

 

 Rais Mpya wa Brazil Michel Temer amesema nchi yake inaingia katika enzi mpya ya matumaini baada ya kuondoshwa madarakani kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff.ENDELEA

 

01.09.2016

Ukuta: Upinzani waahirisha maandamano Tanzania

Muungano wa vyama vya upinzani nchini Tanzania umeahirisha maandamano ya kitaifa ambayo yalikuwa yamepangiwa kufanyika kesho.
Bw Lowassa, ambaye aliwania urais kupitia Chadema katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka 2015
Viongozi wa upinzani, akiwemo Edward Lowassa wa Chadema, wametangaza hatua hiyo kwenye kikao na wanahabari Dar es Salaam.ENDELEA

 

 

 

01.09.2016

Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi Gabon

Ali Bongo atangazwa mshindi wa uchaguzi nchini Bongo

 

Wanachama wa tume ya Uchaguzi mkuu nchini Gabon wametangaza kuwa rais Ali Bongo, amehifadhi kiti chake cha urais baada ya kumshinda mpinzani wake Jean Ping.ENDELEA

 

31.08.2016

Hoja za mwisho kuhusu hatma ya rais Dilma Rousseff

 Rais Rouseff anatuhumiwa kuivunja sheria ya bajeti mwaka 2014,ili kuficha hali mbaya ya kiuchumi inayokabili taifa hilo,tuhuma alizokanusha vikali. Baraza la Senete linatazamiwa leo kusikiliza hoja za mwisho kutoka kwa mawakili wa pande zote mbili, kabla ya kikao cha mwisho ili kufanyika kura hiyo ya kuamua hatma ya rais Rouseff. Kikao hicho kinatazamiwa kuendelea hadi kesho. Ili kumuondoa madarakani rais Rouseff Thuluthi mbili au maseneta 51 miongoni mwa 81 wanapaswa kupiga kura kuunga mkono wazo hilo.ENDELEA

 

 

31.08.2016

Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria

 

 Kundi la wapiganaji la Islamic state limetangaza kuwa mmoja wa kamanda wake mwandamizi ambae ni msemaji wa kundi hilo, Abu Muhammad al-Adnani ameuwawa nchini Syria.ENDELEA

31.08.2016

Viongozi wa upinzani wa Chadema nchini Tanzania kuhojiwa zaidi na polisi

Edward Lowassa ni miongoni mwa watakaofika polisi kuhojiwa zaidi
 Polisi waliwashikilia viongozi hao kufuatia kukiuka amri iliyotolewa na jeshi la polisi mwishoni mwa juma lililopita kupiga marufuku mikutano yote ya ndani ya vyama vya siasa.ENDELEA

 

30.08.2016

Serikali imetangaza kuzifunga stesheni 'zilizomtusi' Magufuli

 Serikali ya Tanzania imetangaza kuzisimamisha kwa muda stesheni mbili za redio ,radio 5 na Magic FM kwa madai ya kumtusi rais Magufuli na kuchochea ghasia nchini.ENDELEA

30.08.2016

Maafisa wa Chadema wakamatwa Tanzania

Polisi nchini Tanzania wamewakamata maafisa wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema akiwemo mgombea wa zamani wa uraiswa chama hicho Edward Lowassa.ENDELEA

 

 

 30.08.2016

Maoni: Kansela Angela Merkel hajaamua juu ya kushiriki katika uchaguzi

 Lakini mgogoro wa wakimbizi tangu mwaka uliopita umebadilisha kila kitu.Hisia miongoni mwa wananchi zimegawanyika. Nusu ya wananchi bado wanamwona Merkel kuwa ni kiongozi mzuri. Lakini wengine wanamkosoa, na hata wanafikia hatua ya kuwa na mtazamo mkali juu yake. ENDELEA

 

30.08.2016

Rais wa Brazil Dilma Rousseff ajieleza baraza la Seneti

Dilma Rousseff akijieleza mbele ya Seneti

 

Nje ya ukumbi wa seneti mamia ya wafuasi wa rais huyo wameonekana wakiendesha magari yao huku wakipiga kelele za kutaka kurudishwa madarakani pamoja na kuwa kuna matumani hafifu kwa Dilma kurejea katika nafasi hiyo. Mmoja kati ya watu wanaoumuunga mkono kiogozi huyo anasemaENDELEA

 

Aug 29, 2016

Mgombea wa upinzani Gabon adai kushinda uchaguzi wa rais

 Ping alisema jana kuwa amechaguliwa na kwamba anamsubiri Rais anayemaliza muda wake amuite na kumpongeza. Jean Ping ameyasema hayo siku mbili kabla ya kutangazwa matokeo rasmi ya uchaguzi wa rais.ENDELEA

 

 29.08.2016

Uchaguzi wa ushindani mkali kuwahi kushuhudiwa Gabon

Mpinzani mkuu Jean Ping.
Wananchi wa Gabon Jumamosi (27.08.2016) wamejitokeza katika uchaguzi atakaokuwa na ushindani mkali kabisa kuwahi kumkabili Rais Ali Bongo ambaye familia yake imeidhibiti nchi hiyo kwa takriban nusu karne.

Bongo mwenye umri wa miaka 57 alishika madaraka hapo mwaka 2009 wakati baba yake Omar alipofariki dunia hapo mwaka 2009 baada ya kuwa madarakani kwa miaka 42 na alisdhinda katika uchaguzi mwaka huo huo.Vyombo vya dola na mitandao iiliyojikita yenye kumpendelea vyote hivyo vikililainishwa na utajiri wa mafuta wa nchi hiyo Bongo yumkini akashinda tena safari hii.ENDELEA

 

 29.08.2016

Uturuki yazidisha mashambulizi ndani ya Syria

 Waasi wanaoungwa mkono na Uturuki wamekabiliana na vikosi vinavyoungwa mkono na Wakurdi kaskazini mwa Syria, huku jeshi la Uturuki likiendeleza kampeni yake ndani ya ardhi ya Syria.
  
Kifaru cha Uturuki kwenye ardhi ya Syria.

Serikali ya Uturuki, ambayo yenyewe inapambana na uasi wa Wakurdi ndani ya ardhi yake, inasema kampeni yake nchini Syria inahusiana pia na kuwazuwia Wakurdi kutwaa maeneo zaidi ndani ya Syria sambamba na kuwarejesha nyuma wapiganaji wa kundi lijiitalo Dola la Kiislamu (IS).

Uturuki inataka kuwazuwia wapiganaji wa Kikurdi kujiimarisha ndani ya Syria karibu na mpaka wake, jambo ambalo inahofia litakipa nguvu chama cha Wakurdi, PKK, ambacho kimekuwa kwenye vita vya miongo mitatu sasa kuwania utawala wake wa ndani.ENDELEA

 

 26.08.2016

Uturuki yazidi kutuma vifaru Syria

Vifaru vyengine kumi vya Uturuki Alhamisi (25.08.2016) vimevuka mpaka kuingia Syria siku moja baada ya wapiganaji wa upinzani wa Syria wanaoungwa mkono na Uturuki kuwatimuwa wanajihadi katika mji wa Jarabulus.
 
 Vifaru hivyo vinatarajiwa kuungana na vile ambavyo vilivuka mpaka hapo jana katika Operesheni Ngao ya Euphrates ambayo Uturuki inasema inakusudia kuwatokemeza wanamgambo wa itikadi kali wa kundi la Dola la Kiislam na wale wa KikurdiENDELEA

 26.08.2016

Colombia yatangaza makubaliano ya kihistoria ya amani

Serikali ya Colombia na waasi wa kundi la FARC wametangaza kufikia makubaliano ya mwisho kumaliza vita vya msituni vilivyodumu kwa miaka 50.Rais Barack Obama amempongeza mwenzake wa Colombia kwa mafanikio hayo.

Kiongozi wa ujumbe wa FARC Ivan Maruez (kushoto) na kiongozi wa ujumbe wa serikali ya Colombia Humberto de la Calle (kulia) wakipeana mikono baada ya kusaini makubaliano ya mwisho mjini Havana. Katikati ni waziri wa mambo ya nje wa Cuba Bruno Rodriguez.
Pande hizo mbili zimesema zimefikia makubaliano kuhitimisha mgogoro na kujenga amani, katika taarifa ya pamoja iliyosomwa na wawakilishi wa Cuba na Norway, ambao ndiyo wapatanishi katika mazungumzo yaliyopelekea kufikiwa makubaliano hayo.ENDELEA

 

 24.08.2016

Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania ataka mazungumzo, upinzani waonya

Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania, jaji mstaafu Francis Mutungi, ameingilia kati mvutano wa vyama vya siasa nchini Tanzania, ambapo ametaka kufanyika kwa kikao cha pamoja kati yake na viongozi wa vyama vya siasa kupata muafaka.
Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania, jaji mstaafu Francis Mutungi
 Uamuzi wa msajili wa vyama kuingilia kati mvutano huu, imekuja baada ya chama kikuu cha upinzani nchini humo, CHADEMA, kusisitiza azma yake ya kufanya maandamano ya nchi nzima September mosi mwaka huu kupinga hatua ya Serikali kukataza kufanya mikutano ya kisiasa.ENDELEA

 

24.08.2016

Majeshi ya Uturuki yaimarisha mashambulizi ngome ya IS, Syria 

 

Kwa siku ya pili mfulululizo majeshi ya Uturuki yameendelea kuyashambulia maeneo ya mpakani yanayodhibitiwa na wapiganaji wa dola la kiislamu IS nchini Syria.
Binali Yildirim:Waziri mkuu wa Uturuki
Hatua hiyo ni katika kuyajibu mashambulizi yanayofanywa na kundi hilo la IS tukio la hivi karibuni likiwa mashambulizi ya makombora mawili yaliyolenga mji wa Karkamis ulio kusini mashariki mwa Uturuki. ENDELEA

 

19.08.2016

Wafuasi 418 wa Ikhwanul Muslimin wahukumiwa adhabu kali na mahakama ya kijeshi ya Misri.

 Mahakama ya kijeshi ya Misri imetoa hukumu ya vifungo vya kuanzia miaka miwili hadi maisha jela kwa watu 418 ambao ni wanachama na wafuasi wa harakati ya Kiislamu ya Ikhwanul Muslimin.


 Mahakama hiyo imetoa hukumu kwa watu 350 bila ya wenyewe kuwepo mahakamani za kuanzia miaka 25 hadi kifungo cha maisha jela. Washtakiwa 68 waliokuwepo mahakamani wamehukumiwa vifungo vya kati ya miaka miwili hadi kumi jela.ENDELEA

 

 19.08.2016

Picha ya mvulana wa Syria iliyowasikitisha wengi

Mvulana Omran mwenye umri wa miaka minne

 

Picha ya mvulana mdogo akiwa ameketi kwenye gari la kubebea wagonjwa Syria, imeweka wazi tena madhila wanayopitia raia nchini Syria.
Mvulana huyo anaonekana akiwa amejaa damu na vumbi baada ya kutekelezwa kwa shambulio la angani mji wa Aleppo.

Picha hiyo ya Omran, 4, imesambaa sana mtandaoni sawa na ilivyofanya picha ya mwili wa Aylan Kurdi, uliopatikana katika ufukwe wa Uturuki mwaka jana.ENDELEA

 

 

19.08.2016

UN:Riek Machar yuko DRC 

 Umoja wa Mataifa umesema Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Kusini Riek Machar ambaye alikuwa haonekana hadharani yuko nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Taarifa zainasema Kikosi cha Majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa yaliyopo Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yalimsaidia yeye, mke wake pamoja na wengine kutoka kwenye mpaka unaogawa nchi hizo mbiliENDELEA

 

 

 

UCHAGUZI WA URAISI ZAMBIA

Edgar Lungu ashinda

Rais wa Zambia Edgar Lungu ametangazwa mshindi wa matokeo ya uchaguzi wa urais kulingana na matokeo rasmi ya uchaguzi.
Tume ya uchaguzi nchini Zambia imesema kuwa Lungu alijipatia asilimia 50.35 siku ya Alhamisi ,ikiwa imepita asilimia 50 inayohitajika ya kuzuia raundi ya pili kulingana na sheria mpya ya uchaguzi. Mpinzani wake Hakainde Hichilemi alijipatia asilimia 47.67 ya kura. Awali,chama chake cha UNPD kilijiondoa katika shughuli ya kuhakiki kura akidai kuwa kulikuwa na udanganyifu.

Posted By: MJOMBA ZECODER

MATUKIO YA KISIASA

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger