Most Popular

Jean Ping wa Gabon kukata rufaa, mahakama ya rufaa

Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Gabon, Jean Ping, amekata rufaa kwenye mahakama ya katiba kupinga matokeo ambapo amesema aliibiwa kura kwenye uchaguzi wa mwezi uliopita. Rais aliyekuwa madarakani Ali Bongo alishinda kuendelea kuongoza nchi hiyo kwa kura chini ya elfu sita. 

Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Gabon, Jean Ping
Ping hakubaliani na matokeo kutoka kwa ngome za bwana Bongo ambapo yeye alishinda kwa zaidi ya asilimia 95 ya kura zote ambapo waliopiga kura walikuwa ni asilimia 99.93. Waangalizi wa umoja wa ulaya nao wamekosoa matokeo kwa baadhi ya majimbo.

Bwana Ping amesema watu kadhaa wameuawa kwenye vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi , lakini serikali imesema kuwa ni watatu pekee ndiyo waliuawa.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Jean Ping wa Gabon kukata rufaa, mahakama ya rufaa

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger