Most Popular

Viongozi wa upinzani wa Chadema nchini Tanzania kuhojiwa zaidi na polisi

Viongozi wa chama cha upinzani cha Chadema Nchini Tanzania walioshikiliwa jana jioni na kuhojiwa na jeshi la polisi na baadaye kuachwa kwa dhamana, wanatarajiwa kurudi tena kikuo kikuu cha polisi leo kwa maojiano zaidi. 

Edward Lowassa ni miongoni mwa watakaofika polisi kuhojiwa zaidi
Viongozi hao walikamatwa jana jioni wakiwa kwenye Hoteli ya Girrafe iliyopo mjijini Dar es salaaam wakifanya mkutano wa ndani ya chama hicho.

Kupanga mikakati ya kutekeleza kile wanachokiita Operasheni Ukuta.
Inayotarajiwa kufanyika septemba mosi ikilenga kupinga kile wanachokiita ni kubanwa kwa demokrasia kwa serikali ya awamu ya tano.

Polisi waliwashikilia viongozi hao kufuatia kukiuka amri iliyotolewa na jeshi la polisi mwishoni mwa juma lililopita kupiga marufuku mikutano yote ya ndani ya vyama vya siasa.

Kufuatia mauaji ya askari polisi wanne yaliyotokea nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Waliokamatwa ni mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, katibu mkuu Dk. Vicent Mashinji, naibu Katibu mkuu bara John Mnyika na makamu mwenyekiti Zanzibar Said Issa
Posted By: MJOMBA ZECODER

Viongozi wa upinzani wa Chadema nchini Tanzania kuhojiwa zaidi na polisi

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger