12.09.2016
Roboti yafanya upasuaji wa macho mara ya kwanza duniani
Mgonjwa kwa jina Bill Beaver mwenye umri wa miaka 70 aliyefanyiwa upasuaji huo sasa anasema anahisi vyema.ENDELEA 
10.09.2016
Galaxy Note 7: Wanaosafiri kwa ndege watahadharishwa
 Kampuni ya Samsung ilisitisha uuzaji wa simu hizo na 
kukubali kwamba kulikuwa na hitilafu wakati wa uundaji wa betri za simu 
hizoENDELEA
09.09.2016
Simu mpya ya Apple iPhone 7 isiyo na headphone za kawaida
![]()  | 
| Apple imesema kuondoa tundu hilo la headphone ya 3.5mm kutanusuru nafasi inayoweza kutumiwa kuongeza vitu vingine | 
Kampuni ya Apple imethibitisha 
kwamba simu yake mpya ya iPhone haitakuwa na tundu la kawaida la kifaa 
cha kusikiza sauti, ambacho kwa Kiingereza hufahamika kama headphone.ENDELEA 
07.09.2016
TV za Sony Bravia kuathiriwa na mabadiliko ya Youtube
 Kutokana na hatua hiyo programu ya You Tube katika runinga hizo itaondolewa  kufikia mwisho wa mwezi huu,Sony imesema.ENDELEA
04.09.2016
CHINA KUFUNGUA DARAJA LA VIOO LILILO JUU YA ARDHI
Daraja la vioo lililojengwa juu nchini Uchina ililosifiwa kwa kuvunja rekodi lilipozinduliwa  siku 13 tu zilizopita limefungwa. ENDELEA
03.09.2016
Samsung yasitisha uuzaji wa Note 7 sababu ya betri
  Mtu mmoja katika YouTube, 
anayesema anaishi Marekani, aliweka mtandaoni video inayoonesha Galaxy 
Note 7 ikiwa imeungua na skrini yake kuharibika.ENDELEA
03.09.2016
Satelaiti ya Facebook ya kufikisha mtandao kasi Afrika yaharibiwa
![]()  | 
| Roketi ya Falcon-9 ilikuwa imeundwa ikiwa na uwezo wa kutua baharini au ardhini ikirejea duniani | 
 Satelaiti
 hiyo kwa jina Amos-Six ilikuwa imebebwa na roketi ya Falcon Nine ambayo
 ililipuka ilipokuwa ikifanyiwa majaribio ya kujiandaa kwa safari ya 
siku ya Jumamosi. 
Mlipuko huo ulitokea wakati roketi hiyo ilikuwa ikijazwa mafuta na kutikiza majengo yaliyokuwa umbali wa kilomita kadha.ENDELEA
Mlipuko huo ulitokea wakati roketi hiyo ilikuwa ikijazwa mafuta na kutikiza majengo yaliyokuwa umbali wa kilomita kadha.ENDELEA
02.09.2016
Acer yazindua laptopu yenye kioo kilichojipinda
 Kampuni ya Acer imezindua laptopu ya
 kwanza ilio na kioo kilichojipinda.Acer inasema kuwa uvumbuzi huo 
utaiwezesha kucheza michezo ya video.ENDELEA
01.09.2016
Rekodi ya kasi ya mtandao wa 4G katika simu yavunjwa
 Kampuni ya Finland Elisa inasema imefanikiwa kupata kasi ya Gigabait 
1.9 kwa sekunde, ikisema hiyo ndio kasi ya juu zaidi kuwahi kupatikana.ENDELEA
29.08.2016
Iran kujenga vinu viwili vipya vya nyuklia
![]()  | 
| Kinu cha nyuklia cha Arak, nchini Iran | 
 Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki
 ya Iran aidha amesema, miswada ya mikataba ya kukifanyia ukarabati wa 
kimsingi kinu cha maji mazito ya nyuklia cha Arak imeshaandikwa. 
Ameongeza kuwa, mikataba hiyo itakuwa na mambo mengi ya kila namna 
ambayo yanahitajia vikao na mazungumzo mbalimbali kuyajadili.ENDELEA
26.08.2016
Japani, Marekani kukuza nishati mbadala Afrika
 Japani na Marekani zimesaini makubaliano juu ya ushirikiano katika kuendeleza uzalishaji wa nishati ya joto ardhi barani Afrika.
Chini ya makubaliano hayo, serikali za nchi hizo mbili zitakuza uwekezaji kwenye vyanzo vya nishati vilivyo rafiki kwa mazingira barani humo. Nchi hizo mbili zitalenga katika maendeleo ya uzalishaji wa nishati ya joto ardhi katika eneo la Afrika Mashariki.
Ni asilimia 30 tu ya watu barani Afrika wanaotumia nishati ya umeme. Kuhakikisha upatikanaji wa vyanzo vipya vya nishati imekuwa ni suala linalohitajika haraka kutokana na uchumi wa eneo hilo kukua. ENDELEA
Chini ya makubaliano hayo, serikali za nchi hizo mbili zitakuza uwekezaji kwenye vyanzo vya nishati vilivyo rafiki kwa mazingira barani humo. Nchi hizo mbili zitalenga katika maendeleo ya uzalishaji wa nishati ya joto ardhi katika eneo la Afrika Mashariki.
Ni asilimia 30 tu ya watu barani Afrika wanaotumia nishati ya umeme. Kuhakikisha upatikanaji wa vyanzo vipya vya nishati imekuwa ni suala linalohitajika haraka kutokana na uchumi wa eneo hilo kukua. ENDELEA
26.08.2016
Sayari inayofanana na Dunia yagunduliwa
Wanasayansi wamegundua sayari ambayo
 inakaribia sana Dunia kwa mazingira na ukubwa wake na ambayo inazunguka
 nyota ijulikanayo kama Proxima Centauri, iliyo na mfumo unaokaribia 
zaidi mfumo wetu wa jua.
![]()  | 
| Proxima Centauri inavyoonekana kwa kutumia darubini ya Hubble Space Telescope | 
Proxima inapatikana umbali wa kilomita trilioni 40 na inaweza kumchukua mtu, akitumia teknolojia ya sasa ya vyombo vya usafiri wa anga za juu, maelfu ya miaka kufika huko.ENDELEA
Simu milioni 900 za Android hatarini
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani. Upungufu huo unaowapa wadukuzi mlango wa nyuma wa kuiga herufi za siri uligunduliwa baada ya watafiti wa hali ya ubora wa programu Checkpoint walipojaribu kusuluhisha hitilafu iliyowezesha kirusi kuambukiza makumi ya mamilioni ya simu zilizokuwa na programu zilizoundwa na kampuni moja ya Marekani QualcommENDELEA











No comments:
Post a Comment