Most Popular

Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria

Kundi la wapiganaji la Islamic state limetangaza kuwa mmoja wa kamanda wake mwandamizi ambae ni msemaji wa kundi hilo, Abu Muhammad al-Adnani ameuwawa nchini Syria. 

Taarifa ya mtandao unaohusiana na kundi hilo Amaq, inasema kuwa Abu Muhammad ameuwawa wakati alipokuwa kwenye operesheni za kijeshi katika jimbo la Allepo.

Abu Muhammad al Adnani
Mtandao huo haukutoa taarifa nyengine zaidi.

Wanajeshi wa marekani wamethibitisha kuwa walikuwa wamemlenga Abu Muhammad al-Adnani lakini wanasema bado walikuwa wakichunguza matokeo ya shambulizi la anga la siku ya Jumanne katika mji wa Al-Bab, kaskazini mashariki ya jimbo la Allepo.

Marekani inamuelezea Abu Muhammad al-Adnani kuwa ni mpangaji mkuu wa mashambulizi ya nje ya I-S na imesema kuwa kifo chake kinaweza kuwa nukta muhimu ya kushindwa kwa kundi hilo.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger