14.09.2016
Wabunge wataka matumizi ya bangi yahalalishwe Uingereza
 Wabunge hao wanataka serikali iondoe bangi kutoka kwa kitengo nambari moja hadi kitengo nambari nne.ENDELEA
12.09.2016
Waislamu kusherehekea Idd-el-Hajj
 Barani Afrika sikukuu hii 
itasherehekea katika nchi mbalimbali, huku baadhi ya nchi zikiwa katika 
hali ya sintofahamu kutokana na makundi yanayodai kuwa yenye msimamo 
mkali wa kidini, hasa nchini Somalia, Nigeria, Mali, Libya, Mauritania 
na nchi nyingine za Kiarabu barani Asia, na Ulaya.
Kati ya Waislamu duniani sikukuu hii hujulikana kwa majina mbalimbali ambayo hutafsiriwa pia kwa lugha mbalimbali kama vile:ENDELEA
Kati ya Waislamu duniani sikukuu hii hujulikana kwa majina mbalimbali ambayo hutafsiriwa pia kwa lugha mbalimbali kama vile:ENDELEA
10.09.2016
Ri Chun-hee:mwanamke maarufu zaidi Korea Kaskazini
Ndiye aliyetangaza vifo vya viongozi wa awali: Kim Il-Sung na Kim Jong-Il.
Ri Chun-hee majuzi alitangaza kufanikiwa kwa Korea Kaskazini kurusha satelaiti ya kuzunguka dunia kwa kutumia roketi. Hilo lilishutumiwa kama njama ya kufanyia majaribio kombora la masafa marefu.ENDELEA
Ri Chun-hee majuzi alitangaza kufanikiwa kwa Korea Kaskazini kurusha satelaiti ya kuzunguka dunia kwa kutumia roketi. Hilo lilishutumiwa kama njama ya kufanyia majaribio kombora la masafa marefu.ENDELEA
09.09.2016
Air China yaomba radhi baada ya kushtumiwa ubaguzi
 Shirika la ndege la China la Air China limeomba 
radhi baada ya kutuhumiwa kujihusisha na mambo ya ubaguzi kwa abiria 
wanaosafiri na ndege zake, na hivyo kulazimika kuondoa gazeti lake 
lililozua utata katika ndege zake.ENDELEA
09.09.2016
Mzee wa umri wa miaka 145 Indonesia
 Mzee huyo anasema kwa sasa anaishiwa na nguvu na hawezi kutarajia aishi muda mrefu zaidi.
"Sina nguvu kama zamani. Hata kutembea ni shida. Nilikuwa mkulima na nilivua samaki mtoni. Sitaki kuendelea kuishi sana, ndio maana nimeandaa kaburi. "Ili nikifariki, kila kitu kiwe tayari," anasema.ENDELEA
"Sina nguvu kama zamani. Hata kutembea ni shida. Nilikuwa mkulima na nilivua samaki mtoni. Sitaki kuendelea kuishi sana, ndio maana nimeandaa kaburi. "Ili nikifariki, kila kitu kiwe tayari," anasema.ENDELEA
05.09.2016
Biashara baina ya nchi za Afrika yasaidia kukuza uchumi
 Licha
 ya kuwa na ukuaji wa wastani wa mauzo ya nje wa asilimia 8.5 tangu 
mwaka 2010, fursa za kibiashara za kikanda hazijatumika kikamilifu 
barani Afrika. 
Hiyo ni kulingana na Ripoti ya hali ya Uchumi wa Afrika ya mwaka 2016 iliyotolewa Jumatano wiki iliyopita. 
Ripoti hiyo inasema, biashara kati ya nchi za Afrika bado ni ya chini ikilinganishwa na sehemu nyingine za dunia.ENDELEA
Ripoti hiyo inasema, biashara kati ya nchi za Afrika bado ni ya chini ikilinganishwa na sehemu nyingine za dunia.ENDELEA
05.09.2016
Mkutano wa kilele wa G20 kusaidia kuharakisha maendeleo ya viwanda Afrika
Mkutano wa 11 wa kilele wa kundi la G20 umefunguliwa leo huko 
Hangzhou, China, ambao umeshirikisha nchi nyingi zaidi zinazoendelea 
katika historia ya kundi la G20. Mkutano huo kwa mara ya kwanza umetoa 
kipaumbele kwa suala la maendeleo kwenye mfumo wa sera za dunia nzima, 
huku ukitoa pendekezo la ushirikiano linalolenga kuunga mkono maendeleo 
ya viwanda wa Afrika na nchi zilizo nyumba kimaendeleo duniani. 
Wachambuzi wanaona kuwa China kuweka ajenda hiyo kwenye mkutano huo na 
kuwaalika nchi za Afrika kuhudhuria mkutano huo kumeonesha kuwa China 
inazingatia suala la maendeleo la nchi za AfrikaENDELEA 
05.09.2016
Utajiri wa Aliko Dangote washuka kwa zaidi ya asilimi 35
  Utajiri wa tajiri mkubwa zaidi barani Afrika raia 
wa Nigeria Aliko Dangote, umeshuka kwa asilimia 35 hadi kufikia kiwango 
cha dola za Marekani bilioni 9.9, kutokana na kushuka kwa thamani ya 
Naira na kuporomoka kwa bei ya madini katika soko la dunia, taasisi ya 
Bloomberg imesema.ENDELEA
04.09.2016
Kirusi cha Zika chahatarisha maisha ya watu bilioni 2 Afrika na Asia
 Uchunguzi umebaini kuwa, kirusi cha Zika 
kinahatarisha maisha ya watu zaidi ya bilioni mbili katika nchi kadhaa 
za mabara ya Afrika na Asia.ENDELEA
03.09.2016
Iran na Tanzania kuimarisha uhusiano wa kiutamaduni
 Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeazimia kuimarisha uhusiano wa kiutamaduni na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.ENDELEA
31.08.2016
Saudi Arabia yafunga sHULE yake Ujerumani
| Skuli ya King Fahd Academy mjini Bonn, Ujerumani, ambayo inamilikuwa na serikali ya Saudi Arabia itafungwa rasmi mwanzoni mwa mwaka 2017. | 
Serikali ya Saudi Arabia imeamua kuifunga shule yake ya pekee nchini 
Ujerumani, baada ya kulalamikiwa kwa muda mrefu kwamba huenda ikawa 
inatumika kupandikiza na kueneza siasa kali.
Ubalozi wa Ufalme wa Saudia mjini Berlin unasema skuli hiyo ifahamikayo kama King Fahd Academy iliyopo katika kiunga cha Bad Godesberg, karibu na mji mkuu wa zamani wa Ujerumani Magharibi, Bonn, itafungwa mwanzoni mwa mwaka ujao.ENDELEA
Ubalozi wa Ufalme wa Saudia mjini Berlin unasema skuli hiyo ifahamikayo kama King Fahd Academy iliyopo katika kiunga cha Bad Godesberg, karibu na mji mkuu wa zamani wa Ujerumani Magharibi, Bonn, itafungwa mwanzoni mwa mwaka ujao.ENDELEA
31.08.2016
IMF: Uchumi wa Tanzania waongoza Afrika Mashariki
 Katika
 ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango 
cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.ENDELEA
30.08.2016
EAC yaidhinisha kiswahili kuwa lugha rasmi
 Bunge la Afrika Mashariki 
limepitisha azimio la kuifanya lugha ya kiswahili kuwa lugha rasmi ya 
jamii ya Afrika Mashariki kulingana na gazeti la The Citizen nchini 
Tanzania.ENDELEA
29.08.2016
Zimbabwe yakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji
| Wanawake na watoto wakisubiri maji mjini Harare | 
 Zimbabwe ambayo zamani ilifahamika kama mzalishaji mkuu wa chakula 
barani Afrika inakumbwa na ukosefu mkubwa wa maji ambao unaweza 
kusababisha na ukame wakati nchi hiyo ikiwa inaelekea katika kipindi cha
 kiangazi.
Kutokana na ukosefu wa maji, wananchi nchini Zimbabwe sasa wanatembea mpaka umbali wa kilometa 15 kufatuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kunywesha mifugo yao kutokana na vyanzo vingi vya maji kukauka, yakiwemo mabwawa na visima.ENDELEA
Kutokana na ukosefu wa maji, wananchi nchini Zimbabwe sasa wanatembea mpaka umbali wa kilometa 15 kufatuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kunywesha mifugo yao kutokana na vyanzo vingi vya maji kukauka, yakiwemo mabwawa na visima.ENDELEA
26.08.2016
Utumwa mambo leo katika ajira
| Wasichana wafanyabiashara nchini Ghana | 
Asilimia 60 ya mataifa yote duniani yapo katika hatari ya kutumia ajira 
ya utumwa mambo leo katika shughuli za uzalishaji licha ya kuwa suala 
hilo la kuwatumikisha watu katika ajira limekuwa likipingwa na 
wanaharakati.
Kulingana na ripoti mpya iliyotolewa hivi karibuni kuhusu viwango vya kutumikishwa watu katika ajira, Korea Kaskazini ndiyo nchi iliyo na rekodi mbaya zaidi ya kutumikisha watu katika ajira.
Utafiti uliofanywa na kampuni ya Verisk Maplecroft ikitumia vigezo vya visa vilivyoripotiwa vya usafirishaji watu kwa njia zisizo halali au utumwaDRC, sheria za nchi na utendaji wa vyombo vya dola katika nchi 198, kampuni hiyo imegundua kuwa nchi 115 ziko katika hatari ya kuwatumia watumwa.ENDELEA
Kulingana na ripoti mpya iliyotolewa hivi karibuni kuhusu viwango vya kutumikishwa watu katika ajira, Korea Kaskazini ndiyo nchi iliyo na rekodi mbaya zaidi ya kutumikisha watu katika ajira.
Utafiti uliofanywa na kampuni ya Verisk Maplecroft ikitumia vigezo vya visa vilivyoripotiwa vya usafirishaji watu kwa njia zisizo halali au utumwaDRC, sheria za nchi na utendaji wa vyombo vya dola katika nchi 198, kampuni hiyo imegundua kuwa nchi 115 ziko katika hatari ya kuwatumia watumwa.ENDELEA
24.08.2016
Hati za umiliki ardhi kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji nchini Tanzania
Nchini Tanzania kumekuwa na mzozo mkubwa wa matumizi ya ardhi baina ya 
wakulima na wafugaji. Lakini juhudi za hivi karibuni za kutoa hati za 
umiliki wa ardhi zinaanza kutoa matunda katika kupunguza mizozo hiyo.
| Mkulima wa mahindi Mkoani Morogoro nchini Tanzania | 
 Hali hii inaelezwa kuchangiwa na uandikishaji duni wa umiliki wa ardhi 
ambao kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na shirika uwazi la kimataifa 
yaani Transparency International 2014 Global Corruption mchakato wa 
upimaji nchini humo meghubikwa na rushwa.ENDELEA
23.08.2016
Madaktari wasio na mipaka kujiondoa Yemen
Shirika la madaktari wasio na mipaka jana lilisema litawaondoa 
wafanyikazi wake kutoka hospitali linazofadhili Kaskazini mwa Yemen 
baada ya watu 19 kuuawa katika shambulizi la angani dhidi ya Hospitali 
moja.
![]()  | 
| Wafanyikazi wa kimataifa wa msaada waondoka Sana'a baada ya uwanja wa ndege wa kimataifa kufunguliwa tena kwa mashirika ya msaada . | 
Muungano unaoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya waasi nchini Yemen hii leo
 umesema kuwa unataka kikao cha dharura na shirika la madaktari 
lisilokuwa na mipaka la -MSF- kuhusiana na hatua ya kutaka kuondoa 
wafanyikazi wake kutoka hospitali sita katika nchi hiyo inayokumbwa na 
ghasia.ENDELEA












No comments:
Post a Comment