Most Popular

Iran kujenga vinu viwili vipya vya nyuklia

Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran amesema, Rais Hassan Rouhani ametoa amri ya kudhaminiwa fedha zinazohitajika kwa ajili ya kujenga vinu viwili vipya vya nyuklia humu nchini.

Shirika la habari la IRNA limemnukuu Bw. Behrouz Kamalvandi akisema hayo jana (Jumapili) mbele ya waandishi wa habari hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, zoezi la ujenzi wa vinu hivyo vipya vya nyuklia litaanza mara baada ya kudhaminiwa fedha zinazotakiwa na kwamba fedha hizo nazo zitapatikana karibuni hivi.

Kinu cha nyuklia cha Arak, nchini Iran
Kamalvandi ameongeza kuwa, wiki mbili zilizopita, ujumbe wa Iran ulielekea nchini China na hivi sasa pande hizo mbili ziko katika mazungumzo kuhusiana na kukifanyia ukarabati wa kimsingi kinu cha nyuklia cha Arak humu nchini.

Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran aidha amesema, miswada ya mikataba ya kukifanyia ukarabati wa kimsingi kinu cha maji mazito ya nyuklia cha Arak imeshaandikwa. Ameongeza kuwa, mikataba hiyo itakuwa na mambo mengi ya kila namna ambayo yanahitajia vikao na mazungumzo mbalimbali kuyajadili.

Aidha amesema, Iran itashirikiana pia na nchi za Ulaya katika miradi yake ya nyuklia, na ushirikiano huo utakuwa zaidi upande wa kudhamini zana na vifaa vinavyohitajika kwa mujibu wa hati rasmi katika nyuga tofauti.

Aidha amesema, washitiri wakubwa wa maji mazito ya nyuklia ya Iran ni nchi za Ulaya na kusisitiza kwamba: Suala la kuiuzia Russia tani 39 za maji hayo liko katika hatua za mwisho na kwamba malipo ya muamala huo yatafanyika kwa sarafu wa euro. Vilevile amesema, hata maji mazito ya nyuklia ya Iran yaliyonunuliwa na Marekani, yamelipwa kwa sarafu ya euro.

Posted By: MJOMBA ZECODER

Iran kujenga vinu viwili vipya vya nyuklia

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger