Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran 
amesema, Rais Hassan Rouhani ametoa amri ya kudhaminiwa fedha 
zinazohitajika kwa ajili ya kujenga vinu viwili vipya vya nyuklia humu 
nchini.
![]()  | 
| Kinu cha nyuklia cha Arak, nchini Iran | 
Kamalvandi ameongeza kuwa, wiki mbili 
zilizopita, ujumbe wa Iran ulielekea nchini China na hivi sasa pande 
hizo mbili ziko katika mazungumzo kuhusiana na kukifanyia ukarabati wa 
kimsingi kinu cha nyuklia cha Arak humu nchini.
Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki
 ya Iran aidha amesema, miswada ya mikataba ya kukifanyia ukarabati wa 
kimsingi kinu cha maji mazito ya nyuklia cha Arak imeshaandikwa. 
Ameongeza kuwa, mikataba hiyo itakuwa na mambo mengi ya kila namna 
ambayo yanahitajia vikao na mazungumzo mbalimbali kuyajadili.
Aidha amesema, Iran itashirikiana pia na
 nchi za Ulaya katika miradi yake ya nyuklia, na ushirikiano huo utakuwa
 zaidi upande wa kudhamini zana na vifaa vinavyohitajika kwa mujibu wa 
hati rasmi katika nyuga tofauti.


No comments:
Post a Comment