Mwanzilishi wa kampuni ya Facebook
Mark Zuckerberg amelezea kusikitishwa kwake baada ya satelaiti ambayo
Facebook ingeitumia kwa mawasiliano ya kasi ya mtandao wa intaneti
barani Afrika kuharibiwa.
![]() |
Roketi ya Falcon 9 ilipolipuka |
Satelaiti hiyo kwa jina Amos-Six ilikuwa imebebwa na roketi ya Falcon Nine ambayo ililipuka ilipokuwa ikifanyiwa majaribio ya kujiandaa kwa safari ya siku ya Jumamosi.
Mlipuko huo ulitokea wakati roketi hiyo ilikuwa ikijazwa mafuta na kutikiza majengo yaliyokuwa umbali wa kilomita kadha.
![]() |
Mfanyakazi katika kituo jirani cha Kennedy Space Center alipiga picha ya mlipuko huo |
![]() |
Roketi ya Falcon-9 ilikuwa imeundwa ikiwa na uwezo wa kutua baharini au ardhini ikirejea duniani |
No comments:
Post a Comment