Most Popular

Biashara baina ya nchi za Afrika yasaidia kukuza uchumi


Biashara baina ya nchi za Afrika yasaidia kukuza uchumi


Licha ya kuwa na ukuaji wa wastani wa mauzo ya nje wa asilimia 8.5 tangu mwaka 2010, fursa za kibiashara za kikanda hazijatumika kikamilifu barani Afrika. Hiyo ni kulingana na Ripoti ya hali ya Uchumi wa Afrika ya mwaka 2016 iliyotolewa Jumatano wiki iliyopita.
Ripoti hiyo inasema, biashara kati ya nchi za Afrika bado ni ya chini ikilinganishwa na sehemu nyingine za dunia.
Biashara baina ya nchi za Afrika ni asilimia 16 ya jumla ya biashara kote barani humo katika mwaka wa 2014 huku bidhaa za viwandani zikichangia asilimia 60 ya biashara ya kikanda barani Afrika.
Mapato ya jumla ya ndani yaani (GDP) kwa miji mikubwa barani Afrika, ikiwa ni pamoja na Johannesburg, Cape Town, Lagos na Luanda, yanatarajiwa kuongezeka, kutokana na ukuaji na ubora wa miundombinu.
Akitoa maoni yake kuhusu ripoti hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa DHL Express katika kanda ya kusini mwa jangwa la Sahara Hennie Heymans alisema, kuna fursa nyingi za kuongeza biashara kati ya nchi za Afrika, hasa kwa kuzingatia manufaa ya makubaliano ya Biashara Huria kati ya jumuiya tatu za kikanda, EAC, SADC na ECOWAS.
Kwa mujibu wa Heymans, nchi ambazo zingetaka kukuza biashara baina yao ni muhimu kufikiria muda na gharama zinazohusiana na usafirishaji wa bidhaa.
Ansema biashara barani Afrika zinaendelea kupata shinikizo katika hali ya sasa ya kiuchumi na kukumbwa na ushindani wa ndani na wa kimataifa na wakati mwingine zinakosa uwezo wa kujenga minyororo imara ya ugavi.
Kwa mujibu wa Heymans, kufanya maamuzi ya kimkakati kuagizia huduma za ugavi kunaweza kuleta mchango muhimu kwa faida ya biashara.
Ikiwa ni bara lenye ukuaji wa kasi zaidi wa tabaka la kati duniani, Afrika ni soko kubwa lenye wateja wanaotafuta upatikanaji rahisi wa bidhaa za aina mbalimbali.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Biashara baina ya nchi za Afrika yasaidia kukuza uchumi

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger