Most Popular

Kirusi cha Zika chahatarisha maisha ya watu bilioni 2 Afrika na Asia

Uchunguzi umebaini kuwa, kirusi cha Zika kinahatarisha maisha ya watu zaidi ya bilioni mbili katika nchi kadhaa za mabara ya Afrika na Asia.

Mtoto aliyeathirika na kirusi cha Zika
Kwa mujibu wa makala iliychapishwa Ijumaa katika jarida la kitiba la 'The Lancet Infectious Diseases' , watu wanaoishi katika nchi zenye watu wengi za Nigeria, India na Indonesia wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kukumbwa na ugonjwa huo hatari. Hii ni kwa sababu wasafiri 5,000 huwasili katika nchi hizo kila mwezi kutoka nchi ambazo zinakabiliwa na mkuripuko wa Zika.
Brazil ndiyo chimbuko la mbu wanaosambaza kirusi cha Zika ambacho sasa kimeenea katika nchi 46 duniani tokea kuibuka kwa mara ya kwanza mwaka 2015

Kirusi hicho pamoja na mambo mengine husababisha wanawake wajawazito kujifungua watoto wenye vichwa vidogo na walio na matatizo ya ubongo.

Add caption
Watu zaidi ya milioni 1.5 nchini Brazil wameambukizwa kirusi hicho na Wizara ya Afya ya nchi hiyo imesema watoto wasiopungua 580 wamezaliwa na maradhi ya microcephaly yanaosababishwa na kirusi cha  Zika.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Kirusi cha Zika chahatarisha maisha ya watu bilioni 2 Afrika na Asia

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger