Most Popular

Zimbabwe yakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji

Zimbabwe ambayo zamani ilifahamika kama mzalishaji mkuu wa chakula barani Afrika inakumbwa na ukosefu mkubwa wa maji ambao unaweza kusababisha na ukame wakati nchi hiyo ikiwa inaelekea katika kipindi cha kiangazi.

Kutokana na ukosefu wa maji, wananchi nchini Zimbabwe sasa wanatembea mpaka umbali wa kilometa 15 kufatuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kunywesha mifugo yao kutokana na vyanzo vingi vya maji kukauka, yakiwemo mabwawa na visima.

Kijana akichota maji katika mto baada ya kumaliza kuoga
Wafugaji na wananchi wa kawaida wanapata wasiwasi kuhofia mifugo yao kufariki na wao kukosa maji ambapo kwa sasa maji hupatikana katika kisima kimoja tu ambacho hutegemewa na kaya zaidi ya 100 na kila familia hupata wastani wa ndoo mbili za lita 20 kwa siku.

Miezi michache iliyopita Zimbabwe ilikubwa na El-Nnino ambayo ilisababisha ukame uliowasababishia takribani watu milioni 4.5 kukabiliwa na ukosefu wa chakula hii, kwa mujibu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP.

El-Nino hiyo ambayo ilikuwa ni kubwa zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 35 illisababisha ukame mkubwa, joto na ukosefu wa maji nchini Zimbabwe.

James Jofirisi mkaazi wa maeneo ya vijijini anasema kumekuwa na uhaba mkubwa wa maji na hata bwawa ambalo hutumika linaweza kukauka muda wowote.

Katika mahojiano yaliyofanyika kwa njia ya simu na waziri wa masuala ya wanawake, jinsia na maendeleo nchini humo amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa Zimbabwe haina suluhisho la tatizo hilo zaidi wanategemea misaada ya wahisani

Nae waziri wa fedha nchini humo Patrick Chinamasa amesema serikali inaweza kusaidia kwa kutoa fedha kupitia mifuko ya maendeleo ya wilaya ili kufanya ukarabati wa visima visivyofanya kazi na kuchimba visima vipya hasa maeneo ya vijiji pamoja na kuwa hajaweka wazi zoezi hilo linaweza kugharimu pesa kiasi gani.


Masuala ya Jamii

Zimbabwe yakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji

Zimbabwe ambayo zamani ilifahamika kama mzalishaji mkuu wa chakula barani Afrika inakumbwa na ukosefu mkubwa wa maji ambao unaweza kusababisha na ukame wakati nchi hiyo ikiwa inaelekea katika kipindi cha kiangazi.
Kijana akichota maji katika mto baada ya kumaliza kuoga
Kutokana na ukosefu wa maji, wananchi nchini Zimbabwe sasa wanatembea mpaka umbali wa kilometa 15 kufatuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kunywesha mifugo yao kutokana na vyanzo vingi vya maji kukauka, yakiwemo mabwawa na visima.
Wafugaji na wananchi wa kawaida wanapata wasiwasi kuhofia mifugo yao kufariki na wao kukosa maji ambapo kwa sasa maji hupatikana katika kisima kimoja tu ambacho hutegemewa na kaya zaidi ya 100 na kila familia hupata wastani wa ndoo mbili za lita 20 kwa siku.
Miezi michache iliyopita Zimbabwe ilikubwa na El-Nnino ambayo ilisababisha ukame uliowasababishia takribani watu milioni 4.5 kukabiliwa na ukosefu wa chakula hii, kwa mujibu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP.
El-Nino hiyo ambayo ilikuwa ni kubwa zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 35 illisababisha ukame mkubwa, joto na ukosefu wa maji nchini Zimbabwe.
Wanawake na watoto wakisubiri maji mjini Harare
James Jofirisi mkaazi wa maeneo ya vijijini anasema kumekuwa na uhaba mkubwa wa maji na hata bwawa ambalo hutumika linaweza kukauka muda wowote.
Wanawake na watoto wakisubiri maji mjini Harare

Misaada ya wahisani inahitajika
Katika mahojiano yaliyofanyika kwa njia ya simu na waziri wa masuala ya wanawake, jinsia na maendeleo nchini humo amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuongeza kuwa Zimbabwe haina suluhisho la tatizo hilo zaidi wanategemea misaada ya wahisani

Nae waziri wa fedha nchini humo Patrick Chinamasa amesema serikali inaweza kusaidia kwa kutoa fedha kupitia mifuko ya maendeleo ya wilaya ili kufanya ukarabati wa visima visivyofanya kazi na kuchimba visima vipya hasa maeneo ya vijiji pamoja na kuwa hajaweka wazi zoezi hilo linaweza kugharimu pesa kiasi gani.

Zimbabwe ni moja kati ya nchi ambazo ziliathiriwa zaidi na El-Nino hasa katika maeneo ya Manicaland, Masgingo, Mertebeleland kusini na kaskazini

Posted By: MJOMBA ZECODER

Zimbabwe yakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger