Most Popular

Wazayuni wakiri wajibu wa kuundwa nchi huru ya Palestina

Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD amesema, suala la kuundwa nchi huru la Palestina ni jambo lisiloepukika.

Tamir Pardo, mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD
Shirika la habari la Associated Press limemnukuu Tamir Pardo akisema hayo jana na kuongeza kuwa, suala la kuanzishwa nchi huru ya Palestina ni muhimu mno kwa usalama wa Mashariki ya Kati.
Matamshi hayo ya mkuu wa zamani wa shirika la kijasusi la utawala wa Kizayuni limeongeza idadi ya maafisa wa masuala ya usalama wa Israel ambao wanaamini kuwa amani haiwezi kupatikana Mashariki ya Kati bila ya kuundwa nchi huru ya Palesitna

Tamir Pardo amesema: Israel haiwezi kufikia makubaliano yoyote ya maana na ulimwengu wa Kiarabu bila ya kutatua kwanza kadhia ya Palestina

Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD amesema, suala la kuundwa nchi huru la Palestina ni jambo lisiloepukika.
Pia amesema, Benjamini Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni amepasisha pendekezo la kuundwa nchi huru ya Palestina, lililobakia sasa ni kumtaka atekeleze kivitendo tu pendekezo hilo.
Makumi ya makamanda wa zamani wa kijeshi na kiusalama wa Israel wamemtaka Benjamin Netanyahu afanye juhudi kubwa zaidi za kulipatia ufumbuzi suala la Palestina.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Wazayuni wakiri wajibu wa kuundwa nchi huru ya Palestina

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger