Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD amesema, suala la kuundwa nchi huru la Palestina ni jambo lisiloepukika.
Tamir Pardo, mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD |
Shirika la habari la Associated
Press limemnukuu Tamir Pardo akisema hayo jana na kuongeza kuwa, suala
la kuanzishwa nchi huru ya Palestina ni muhimu mno kwa usalama wa
Mashariki ya Kati.
Matamshi hayo ya mkuu wa zamani wa
shirika la kijasusi la utawala wa Kizayuni limeongeza idadi ya maafisa
wa masuala ya usalama wa Israel ambao wanaamini kuwa amani haiwezi
kupatikana Mashariki ya Kati bila ya kuundwa nchi huru ya Palesitna
Tamir Pardo amesema: Israel haiwezi
kufikia makubaliano yoyote ya maana na ulimwengu wa Kiarabu bila ya
kutatua kwanza kadhia ya Palestina
![]() |
Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD amesema, suala la kuundwa nchi huru la Palestina ni jambo lisiloepukika. |
Pia amesema, Benjamini Netanyahu, Waziri
Mkuu wa utawala wa Kizayuni amepasisha pendekezo la kuundwa nchi huru
ya Palestina, lililobakia sasa ni kumtaka atekeleze kivitendo tu
pendekezo hilo.
Makumi ya makamanda wa zamani wa kijeshi
na kiusalama wa Israel wamemtaka Benjamin Netanyahu afanye juhudi kubwa
zaidi za kulipatia ufumbuzi suala la Palestina.
No comments:
Post a Comment