Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa,
jumla ya watu 500 wamepoteza maisha yao nchini Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo, kutokana na ugonjwa wa kipindupindu.
![]() |
Mgonjwa wa kipindupindu akiwahishwa hospitali |
Ni vyema kuashiria kuwa, maradhi ya kipindupindu yamekuwa yakiripuka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hususan katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa duru za afya nchini humo tangu mwezi Agosti hadi sasa watu 13 wameambukizwa ugonjwa huo mjini Kinshasa, mji mkuu wa taifa hilo, huku wawili wakiripotiwa kufariki dunia. Ugonjwa wa kipindupindu huambukiza kutokana na kunywa maji yasiyo salama ambapo huendana na mgonjwa kuharisha na kutapika.
No comments:
Post a Comment