Walanguzi wawili wa biringanya raia
wa Burundi wameuawa jana usiku upande wa Rwanda wa mpakani, kwa mujibu
wa msemaji wa polisi wa Burundi, Pierre Nkurikiye.
![]() |
Wafanya biashara wa bringanya wa Burundi wameathiriwa sana |
Mwezi Julai, Burundi ilipiga marufuku usafiri wa umma na biashara zozote za chakula na Rwanda kwa sababu za kiusalama.
Wakulima wa biringanya na nyanya katika mkoa wa kaskazini magharibi mwa Burundi wa Cibitoke wameathirika pakubwa na uamuzi huo kwani Rwanda lilikua soko kuu la bidhaa zao.
Uhusiano baina ya Burundi na Rwanda umekuwa ukiendelea kuzorota tangu mwaka jana , huku serikali ya Bujumbura iskishutumu serikali ya Kigali kuwahifadhi waliopanga njama ya mapinduzi ya mwaka 2015 na kutoa zana na mafunzo ya kijeshi kwa warundi wanaoishi kambini nchini Rwanda.
Rwanda inapinga shutuma hizo inazosema hazina msingi wowote.
No comments:
Post a Comment