Most Popular

UN yatishia kuichukulia hatua Korea Kaskazini

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu siku ya Jumatatu.


Pyongyang ilirusha makombora matatu baharini mkutano wa viongozi wa mataifa 20 yenye ushawishi mkubwa duniani ulipokuwa ukiendelea nchini China.

Kwenye azimio lililopitishwa kwa kauli moja na wanachama 15 wa baraza hilo, ikiwemo China - mshirika mkuu wa Korea Kaskazini - baraza hilo lilitishia kuchukua "hatua nyingine kali" dhidi ya taifa hilo lisipositisha majaribio ya mabomu ya nyuklia na makombora.

Korea Kaskazini imezuiwa na UN kutekeleza majaribio hayo na imekuwa ikiwekewa vikwazo mara kwa mara.
Posted By: MJOMBA ZECODER

UN yatishia kuichukulia hatua Korea Kaskazini

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger