Mshambuliaji nyota wa kimataifa wa 
Tanzania, Mbwana Samatta leo anatarajiwa kuingoza klabu yake ya KRC Genk
 ya Ubelgiji katika mchezo wa marudiano wa mwisho kuwania nafasi ya 
kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya Europa League dhidi ya Lokomotiva
 Zagreb ya Croatia .
![]()  | 
| Samatta alianza kuchezea timu ya taifa ya Tanzania 2011 | 
Wakifanikiwa, basi Samatta atapata nafasi ya kucheza katika hatua ya makundi Europa League.
Katika mchezo uliopita Samatta ambaye pia ni nahodha wa taifa Stars, alifunga bao katika sare hiyo iliyopatikana na wanakwenda katika mchezo huo wakiwa wametoka kushinda mchezo wao ligi ya Ubelgiji kwa mabao 3-0 Jumapili iliyopita huku Samatta akifunga mabao mawili kati ya hayo.
Kama Genk wakifanikiwa kupata sare ya bila mabao au ushindi mwembamba kuanzia 1-0 moja kwa moja watakuwa wametinga hatua inayofuata ya makundi ambayo ratiba yake inatarajiwa kupangwa Ijumaa


No comments:
Post a Comment