Most Popular

Naibu rais azindua kondomu zenye ladha Afrika Kusini

Naibu wa rais nchini Afrika Kusini alichukua fursa bungeni wakati ambapo rais wa taifa hilo Jacob Zuma alikuwa amesafiri nje ya nchi kuwakilisha maswala ya serikali ikiwemo kondomu isiyo na kelele na yenye ladha ya machungwa kwa wabunge.

Naibu rais nchini Afrika Kusini Cyril Ramaphosa akizundua mipira ya Kondomu bungeni
Cyril Ramaphosa alielezea kwamba mipira hiyo ya kondomu ilitengezwa kufuatia malalamishi kwamba kondomu za serikali zilikuwa zina harufu mbaya na kelele.

Tangazo hilo la Ramaphosa lilizua hasira na tabasamu kutoka wanachama wa ANC na kelele kutoka kwa upinzani wa chama cha EFF huku baadhi ya wanachama wake wakisema ''mpatie Zuma hizo''.

Matamshi hayo ya wanachama wa EFF yanatoka miaka 10 iliopita wakati bwana Zuma alipokiri kwamba katika kesi yake ya ubakaji ,alifanya mapenzi bila kutumia mipira ya kondomu na mwanamke aliyekuwa na virusi vya HIV.

Aliondolewa mashtaka hayo lakini kukiri kwake kulizua mshangao mkubwa nchini humo ambapo takriban watu milion saba wana virusi
Posted By: MJOMBA ZECODER

Naibu rais azindua kondomu zenye ladha Afrika Kusini

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger