Most Popular

Mark Zuckerberg ala ugali Kenya

Mwanzilishi wa kampuni ya facebook Mark Zuckerberg amezuru nchini Kenya katika ziara yake ya mataifa ya bara Afrika.

Mark Zuckerberg akila Ugali na samaki nchini Kenya
Zuckerberg aliyewasili siku ya Jumatano kutoka nchini Nigeria alifanya kikao na waziri wa habari nchini Kenya Joseph Mucheru,ambapo walizungumza kuhusu mtandao na mipango ya serikali kuhakikisha kila kijiji kimeunganishwa na mtandao.

Baadaye Zuckerbag aliekea katika hoteli ya Mama Oliech katika chakula cha mchana ambapo kwa mara ya kwanza alikula Ugali na Samaki.

''Swala muhimu ninapozuru taifa lolote jipya ni kujaribu kula chakula chao.Nilipenda sana ugali na samaki mzima wa tilapia'',alisema Zuckerberg.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Mark Zuckerberg ala ugali Kenya

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger