Vikosi vya uokoaji vya majini vya 
Italy vimesema vimeratibu uokoaji wa wahamiaji elfu sita na mia tano 
katika bahari ya Mediterania siku ya jumatatu. Kwa mujibu wa vikosi 
hivyo, hii ni oparesheni kubwa zaidi kuwahi kutokea katika miaka ya hivi
 karibuni. 
![]()  | 
| Mmoja wa wahamiaji akimbeba mtoto wake wa siku tano kuelekea katika boti ya waokoaji | 
Maelfu ya raia wa kiafrika, wengi wao wakitafuta maisha bora barani ulaya, mara nyingi husafirishwa katika madau ambayo hayana hadhi ya kuhimili mikiki mikiki ya bahari.
Katika msafara huo pia, kuna wakimbizi kutoka maeneo ya vita kama mashariki ya kati na Afghanistan. Wengi wao wamepoteza maisha yao.


No comments:
Post a Comment