Kiungo wa kati wa Chelsea Cesc Fabregas amepinga madai kwamba alikosana na meneja wa klabu hiyo Antonio Conte.
| Cesc Fabregas | 
Fabregas hatahivyo amechapisha katika mitandao ya kijamii akisema kuwa wawili hao wana uhusiano mzuri na kwamba ataendelea kuichezea Chelsea.
''Mbali na ilivyoandikwa, mkufunzi Conte hajawahi kuniambia kwamba niondoke '',aliandika Fabregas.
| Mkufunzi wa Chelsea Conte | 
''Aliniambia kwamba ananitegemea na mimi namtegemea.Nitaendelea kuichezea klabu hii hadi mwisho na iwapo nitahitajika nitajitolea''

No comments:
Post a Comment