Most Popular

Fabregas akana kukosana na mkufunzi Conte

Kiungo wa kati wa Chelsea Cesc Fabregas amepinga madai kwamba alikosana na meneja wa klabu hiyo Antonio Conte.

Meneja huyo aliripotiwa kumtaka mchezaji huyo wa miaka 29 kuondoka kabla ya kukamilika kwa siku ya mwisho ya uhamisho.
Cesc Fabregas

Fabregas hatahivyo amechapisha katika mitandao ya kijamii akisema kuwa wawili hao wana uhusiano mzuri na kwamba ataendelea kuichezea Chelsea.

''Mbali na ilivyoandikwa, mkufunzi Conte hajawahi kuniambia kwamba niondoke '',aliandika Fabregas.
Mkufunzi wa Chelsea Conte

''Aliniambia kwamba ananitegemea na mimi namtegemea.Nitaendelea kuichezea klabu hii hadi mwisho na iwapo nitahitajika nitajitolea''
Posted By: MJOMBA ZECODER

Fabregas akana kukosana na mkufunzi Conte

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© WWH-WORLD WIDE HABARI All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger