Bunge nchini Uganda linatarajiwa kutumia Dola za
Marekani 177,000 kuwatuza medali wabunge 1,200 waliohudumu katika bunge
la nchi hiyo kati ya mwaka 1962 hadi 2012.
![]() |
Lango la kuingilia Bunge la Uganda jijini Kampala |
Vyombo vya Habari nchini humo
vinaripoti kuwa sherehe za kuwatuza wabunge hao zitafanyika mwishoni mwa
mwezi huu katika maadhimisho ya miaka 50 ya bunge hilo.
Kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye na mkewe Winnie Byanyima ni miongoni mwa wabunge wa zamani watakaopata medali hizo.
Raia wa Uganda, wameonekana wakipinga matumizi ya fedha hizo katika sherehe hizo wakati huu raia wa nchi hiyo wakiendelea kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi.
Hatua hii imekuja baada ya Gazeti la serikali ya New Vision kutangaza kuwa bunge limepanga kutumia fedha hizo kufanikisha shughuli hiyo.
Wabunge 13 wamefariki dunia kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye na mkewe Winnie Byanyima ni miongoni mwa wabunge wa zamani watakaopata medali hizo.
Raia wa Uganda, wameonekana wakipinga matumizi ya fedha hizo katika sherehe hizo wakati huu raia wa nchi hiyo wakiendelea kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi.
Hatua hii imekuja baada ya Gazeti la serikali ya New Vision kutangaza kuwa bunge limepanga kutumia fedha hizo kufanikisha shughuli hiyo.
Wabunge 13 wamefariki dunia kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
No comments:
Post a Comment